• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Bukoba Municipal Council
Bukoba Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Ardhi na Mipango miji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo Uwekezaji
    • Ufugaji Uwekezaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayotekelezwa
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
      • Mfuko wa Afya
      • Kodi ya Majengo
      • Hati Rasmi
    • Mpango Mkakati
      • Ripoti Mbalimbali
        • Council Annual Report
          • Kituo cha Habari
            • Taarifa kwa Umma
            • Video za shughuli za Ofisi/Kitaifa
            • HOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB.)
        • Quarterly Financial Report
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu Mbalimbali
      • Leseni ya Biashara
      • Fomu ya uadilifu
      • Fomu ya OPRAS
    • Ripoti Mbalimbali
      • Council Annual Report
        • Kituo cha Habari
          • Taarifa kwa Umma
          • Video za shughuli za Ofisi/Kitaifa
          • HOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB.)
      • Quarterly Financial Report
    • Miongozo mbalimbali
      • Kanuni za Uchaguzi
      • Mwongozo wa Kuendesha Tovuti
      • Mwongozo wa Matumizi Bora, Sahihi na Salama ya Vifaa na Mifumo ya TEHAMA Serikalini
    • Bukoba MC Profile
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • HOTUBA YA MHESHIMIWA KASSIM M. MAJALIWA (MB.)

MAENDELEO YA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI IHUNGO

Posted on: September 13th, 2018

1.0: Utangulizi:

Shule ya Sekondari Ihungo ilianza Mwaka 1947 ikiwa na namba ya usajili S.41. Shule hii ilikuwa na uwezo wa kudahili wanafunzi mia sita (600) kwa kidato cha kwanza hadi cha sita. Miundombinu ya shule ni pamoja na vyumba vya madarasa kumi na nne (14), Nyumba za walimu ishirini (20),Vyumba vya maabara vitatu ( 03),Mabweni sita (06), Matundu ya vyoo thelathini na mbili (32),Jengo moja  la Utawala (01), Chumba cha maktaba kimoja (01), Jengo moja la kompyuta (01), Kanisa na msikiti mmoja (01).

2.0: Athari za tetemeko:
Shule hii ni mojawapo ya taasisi zilizoathiriwa na tetemeko la ardhi lililotokea tarehe 10/09/2016 mkoani Kagera.  Miundombinu yote ya shule iliathirika na tetemeko hili ikiwemo Vyumba vya madarasa, mabweni, vyumba vya maabara,bwalo,vyoo, nyumba za walimu, Jengo la utawala, kanisa, msikiti na miundombinu ya umeme.

3.0: Juhudi za kurejesha miundombinu:
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanya jitihada za makusudi za kurejesha hali ya miundombinu pamoja na kuiboresha zaidi kama ifuatavyo:-

  •  Madarasa:
    Serikali imejenga majengo matatu (03) makubwa ya ghorofa yenye vyumba nane (8) vya madarasa na vyumba vitatu vya ofisi kwa kila jengo moja.  Jumla ya majengo matatu yenye vyumba vya madarasa (24) vyenye uwezo wa wanafunzi 45 kila mmoja.
  •  Ofisi za walimu
    Majengo matatu ya madarasa kila moja lina vyumba vitatu vya ofisi za walimu na kufanya jumla ya vyumba vya ofisi kuwa (12) vyenye uwezo wa kutumiwa na walimu zaidi ya kumi kwa kila chumba kimoja.
  •  Mabweni ya wanafunzi
    Serikali imejenga majengo mawili (02) makubwa ya ghorofa mbili (2) kila moja, kila jengo lina uwezo wa kuchukua wanafunzi (384) jumla ya wanafunzi katika majengo haya ni 1,152.
  • Nyumba za wafanyakazi/walimu
    Serikali inajenga nyumba za wafanyakazi kwa ajili ya familia thelathini (30) ambazo zipo katika hatua mbalimbali za ukamilishaji.
  • Ukarabati
    Majengo yaliyofanyiwa ukarabati ni pamoja na jengo la utawala, maabara ya Kompyuta, jengo la kilimo,bwalo na maabara za Fizikia, Kemia na Baolojia.

4.0: MATENGENEZO YA SAMANI

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilitoa Tshs 623,130,000 kwa ajili ya matengenezo ya samani za shule kwa ajili ya kujiandaa kupokea wanafunzi.                                                        Baadhi ya vifaa vilivyotengenezwa/vilivyopokelewa shuleni  kwa awamu ya kwanza ni pamoja.

Na
Samani/vifaa
Mahitaji
Vilivyokamilika
1
Meza za wanafunzi
1152
892
2
Viti vya darasani
1152
809
3
Viti vya bwaloni
1152
200
4
Vitanda (deka)
576
403
5
Vyungu
18
18
6
Madishi ya Chakula
192
50
7
Meza za bwaloni
200
25


Matengenezo ya samani/vifaa katika awamu ya kwanza bado yanaendelea ili kuweza kukamilisha idadi ya mahitaji yaliyoainishwa hapo juu.  Katika awamu ya pili shule itatengeneza samani zifuatazo: 

vifaa vinavyotengenezwa/vitakavyopokelewa shuleni  kwa awamu ya pili

Na
Samani
Mahitaji
1
Kabati za bwaloni
4
2
Kabati za bwenini
1152
3
Kabati za ofisini
3
4
Kasiki
1
5
Meza za Maktaba
100
6
Meza za walimu
123
7
Shubaka
17
8
Viti vya Maktaba
600
9
Viti vya walimu
174


5.0 Mapokezi ya kidato cha Tano:
Shule ilipangiwa wanafunzi 679 ambao walianza kuripoti shuleni tarehe 16/7/2018 mpaka sasa wanafunzi walioripoti ni 556 katika tahsusi  za PCB, PCM, CBF,EGM na HGE  na masomo yanaendelea kulingana na  ratiba ya shule.


6.0      MAFANIKIO:    

  1.   Shule imeweza kufanya vizuri katika taaluma kwa mwaka 2017 na 2018 katika mitihani ya kidato cha sita na changamoto za tetemeko la ardhi zilizosababisha kuhama.
  2. Jitihada za serikali ya awamu ya tano zimefanikisha, miundombinu ya shule kujengwa upya na uwezo wa shule umeongeza kutoka wanafunzi 600 kabla ya tetemeko hadi 1,152 baada ya tetemeko.  
  3. Idadi ya nyumba za walimu imeongezeka kutoka nyumba ishirini(20) zilizokuwepo awali kufikia nyumba arobaini na saba (47) za sasa.
  4. Serikali imetoa fedha ambazo zimeboresha miundo mbinu ya samani ambapo kila mwanafunzi amepata dawati lake na kitanda pamoja na miundombinu mengine kama makabati n.k.









Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUFUNGULIWA KWA DIRISHA LA KUOMBA MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA NA HALMASHAURI KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU March 22, 2025
  • TERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN BUKOBA MUNICIPALITY UNDER THE TACTIC PROJECT March 10, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI February 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA YA BUKOBA February 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "HATIBU OR-TAMISEMI: "TUENDELEE KUFUATILIA NA KUSIMAMIA MIRADI YETU KWA UKARIBU"

    May 27, 2025
  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • DC. SIMA AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA MKATABA WA LISHE NGAZI YA KATA MANISPAA YA BUKOBA

    May 10, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI ASISITIZA UTUNZWAJI WA VIFAA VYA UANDIKISHAJI.

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba akitoa maelezo juu ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2023/2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miradi ya Mbalimbali
  • Nyaraka mbalimbali
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Tovuti kuu ya Takwimu Huria

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bukoba Municipal Coucil

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 284 Bukoba

    Telephone: +255 28 2220226

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@bukobamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2017 Manispaa ya Bukoba .Haki zote Zimehifadhiwa